Jumatatu, 4 Julai 2016

Ajali iliyohusisha magari 2 ya City Boy yamegongana nakuua

Singida. Watu 29 wamefariki dunia na wengine kujeruhiwa leo baada ya mabasi mawili kugongana huko Maweni wilayani Manyoni Mkoa Singida.



Mabasi hayo yanayomilikiwa na Kampuni ya City Boy, moja lilikuwa linasafiri kutoka Dar es Salaam kwenda Kahama na lingine lilikuwa linatoka Kahama kwenda Dar es Salaam.
Akizungumzia ajali hiyo, Kamanda wa Polisi mkoani Singida, Thobias Sedoyeka amesema idadi ya majeruhi bado haijajulikana japo kuwa amesema ni wengi.
"Nikweli ajali imetokea Maweni na tupo eneo la tukio tunaendelea na utaratibu wa kuondoa majeruhi na maiti," amesema Kamanda


Jumapili, 12 Juni 2016

Rais afanya mabadiliko Baraza la mawazili

Dar es Salaam.



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk John Magufuli amefanya mabadiliko madogo katika Baraza la Mawaziri huku akimteua Mbunge wa Buchosha Dk. Charles Tizeba kuwa Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi.

Kufuatia uteuzi huo, aliyekuwa Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi Mwigulu Nchemba ameteuliwa kuwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi.

Nchemba anachukua nafasi iliyoachwa wazi na aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Charles Kitwanga ambaye uteuzi wake ulitenguliwa.

Mawaziri walioteuliwa katika mabadiliko hayo wataapishwa Jumatatu  asubuhi Ikulu jijini Dar es Salaam.


Ijumaa, 20 Mei 2016

#HABARI Rais atengua uteuzi wa wazili wa mambo ya ndani

Rais‬wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli ametengua uteuzi wa Waziri wa Mambo yaNdani ya Nchi, Mheshimiwa Charles Kitwanga kuanzia leo tarehe 20 Mei, 2016.Rais Magufuli ametengua uteuzi huo kufuatia kitendo cha Mheshimiwa Charles Kitwanga kuingia bungeni na kujibu swali linaloihusu wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi akiwa amelewa.

Jumatano, 18 Mei 2016

Vanessa na shilole bado kizungu mkut

Zilianza kuandikwa siku ya May 17 2016 baada ya mastaa wawili kutoka kiwanda cha bongoflevani kurushiana maneno katika post zao walizozipost kwenye mtandao wa Instagram, Stori ilianzia kwenye Picha, lakini this time kila moja ameongea.Baada ya Shilole na Vanessa Mdee kurushiana Maneno kupitia Picha zao kila mmoja kwa time yake amezungumza na nakufunguka haya..Vanessa Mdee alifunguka maneno haya>>Nadhani nimeshasema kilakitu ambacho kinahitaji kusemwa kama umesoma post yangu utakuwaumeshaelewa kama hujasoma sawa sihitaji kurudia kitu’Shilole na yeye kuyafunguka haya>>’acha nimnyooshe kapanic kuona Say my name imetoka na mimi kuzinguliwa sitaki kuna mahalikaenda kuniongelea vibaya na asitamani kuonana na Shishi atatamani kuadithia vibao nilivyokuwa natoa somewhere

posted from Bloggeroid

Ijumaa, 13 Machi 2015

Faida ya juisi ya ukwaju

Ukwaju ni tunda lenye faida nyingi sana kwa afya ya mwanadamu.

Ukwaju ni tunda lenye faida nyingi sana kwa afya ya mwanadamu. Tunda hili   linatumika kutengeneza juisi ambayo matumizi yake yana faida kubwa sana  kiafya.


Faida ya juisi ya ukwaju

Hushusha joto la mwili na kuondosha homa, hasa homa ya matumbo .

Huulinda mwili dhidi ya mafua 

Husaidia myeyusho na mmengenyo wa chakula
 
Husaidia kutibu matatizo ya nyongo  

Husaidia kurahisisha choo (laxative)

Husaidia kupunguza wingi wa lehemu (cholesterol) na  kuimarisha moyo 

Husaidia ngozi kuwa nyororo,
 
Husaidia kuua minyoo tumboni (kwa watoto wadogo)

kwa wanaofanyiwa oparation ni nzuri sana inakausha kidonda kwa ndani kwa haraka . 


Jumatano, 11 Machi 2015

Watu 40 wamepoteza maisha kwajali ya gali mkoani iringa

Watu 41 wamefariki katika eneo la Changarawe, Mafinga mkoani Iringa,nyanda za juu kusini mwa Tanzania, baada ya basi la kampuni ya Majinja Express walilokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na Lori.
Miili ya waliofariki katika ajali hiyo imepelekwa hospitali ya Mafinga mkoani humo.
Kamanda wa polisi mkoani Iringa Ramadhani Mvungi amethibisha kutokea kwa ajali hiyo na kusema kuwa kati ya hao 41 waliopoteza maisha,wanaume ni 33,wanawake watano na watoto watatu.
Akielezea chanzo cha ajali hiyo, Kamanda Mvungi amesema kuwa dereva wa Lori alijaribu kukwepa moja ya shimo katika barabara swala lililomsababisha kutoka katika upande wake wa barabara hadi upande wa basi hilo na kusababisha kugongana uso kwa uso.


Hata hivyo kasha la lori hilo liliangukia basi hilo la kampuni ya Majinja na kusababisha vifo kwa abiria hao.
Miili ya waliofariki katika ajali hiyo imehifadhiwa katika hospitali ya Mafinga mkoani humo,na majeruhi wanaendelea kupatiwa matibabu katika hospitali hiyo.
Kwa mjibu wa kamanda mvungi taarifa zaidi zitaendelea kutolewa kuhusiana na ajali hiyo.
Kumekuwa na ajali za mara kwa mara za barabarani katika nchi za Afrika mashariki ambazo husababishwa na mwendo wa kasi wa madereva na ubovu wa barabara.


Jumapili, 8 Machi 2015

#MICHEZO Manchester United kumuuza Di Maria

Di Maria hajaonyesha umahiri wake tangu aliposajiliwa katika kilabu ya Manchester united kutoka Real Madrid na inaaminika kwamba yeye na mkewe hawajazoea maisha ya Manchester baada ya jaribio la wizi katika nyumba yao.
Wiki iliopita raia huyo wa Argentina ,mkewe Jorgelina Cardoso na mwanawe wa mwaka mmoja wamehamia katika nyumba ya aliyekuwa mchezaji wa Manchester United Phil Nevile iliopo ghorofa ya 45.
Wamekodisha nyumba hiyo kwa kuwa Di Maria ana mpango m'badala wa maisha yake swala ambalo kilabu ya Manchester United inalifahamu.


Hatua hiyo inadaiwa kushinikiza harakati za kilabu hiyo kutaka kumsajili mchezaji wa Real Madrid Gareth Bale.
Ijapokuwa Bale amekuwa akisema kuwa hataki kuondoka katika kilabu ya Real Madrid ili kurudi katika ligi ya Uingereza,United inahisi kwamba inaweza kum'bembeleza ili kubadilisha msimamo wake iwapo watakubaliana na mabingwa hao wa Ulaya.