Ijumaa, 13 Machi 2015

Faida ya juisi ya ukwaju

Ukwaju ni tunda lenye faida nyingi sana kwa afya ya mwanadamu.

Ukwaju ni tunda lenye faida nyingi sana kwa afya ya mwanadamu. Tunda hili   linatumika kutengeneza juisi ambayo matumizi yake yana faida kubwa sana  kiafya.


Faida ya juisi ya ukwaju

Hushusha joto la mwili na kuondosha homa, hasa homa ya matumbo .

Huulinda mwili dhidi ya mafua 

Husaidia myeyusho na mmengenyo wa chakula
 
Husaidia kutibu matatizo ya nyongo  

Husaidia kurahisisha choo (laxative)

Husaidia kupunguza wingi wa lehemu (cholesterol) na  kuimarisha moyo 

Husaidia ngozi kuwa nyororo,
 
Husaidia kuua minyoo tumboni (kwa watoto wadogo)

kwa wanaofanyiwa oparation ni nzuri sana inakausha kidonda kwa ndani kwa haraka . 


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni