Watu 42 wamepoteza maisha na wengine 82
kujeruhiwa baada ya mvua ya upepo mkali
kusababisha mafuriko katika kata ya mwakata
wilayani Kahama mkoani Shinyanga.
Mvua hiyo ambayo ilinyesha kwa muda mfupi
imewaacha watu 3,500 bila makazi katika kaya
350 huku nyumba zikifurika maji na baadhi ya
mifugo ikisombwa.
Mkuu wa mkoa wa Shinyanga Bw. Ali Nasoro
Rufunga amesema mvua hiyo ya mawe
iliyoambatana na upepo mkali ilisababisha
mafuruko katika kata ya Mwakata kuezua nyumba
na nyingine kuanguka.
Amesema mali mbalimbali zimeharibiwa vibaya
ikiwemo mifugo kuzolewa na maji na vyakula
kwenye eneo lote lililokumbwa na mafuriko hayo.
Hali ya majeruhi ambao wamepelekwa katika
hospitali mbalimbali bado sio nzuri kwa baadhi
ingawa wengine wanaendelea vizuri.
Jumatano, 4 Machi 2015
Watu 42 kupoteza maisha na 82 kujeluhiwa kutokana na mvua kali na upepo mkali kusababisha mafuliko
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni