Ijumaa, 20 Februari 2015

Breaking news

kwa tasnia ya muziki wa kizazi kipya
nchini.
Mwanamuziki wa kizazi kipya nchini Tanzania
Moses Bushagama maarufu kwa jina la Mez B
ambaye alikuwa muimbaji katika kundi la Chamber
Squard,inaelezwa kuwa amefariki Dunia leo asubuhi
wakati amelazwa katika hospitali ya mwananchi
mjini Dodoma akipatiwa matibabu.
Akizungumza baada ya kupigiwa simu Dada wa Mez
B amethibitisha kifo cha kaka yake ambapo
amesema ni muda hivi amekuwa akisumbuliwa wa
homa pamoja na tatizo la kuishiwa Damu na hivyo
walimpeleka katika hospitali ya GENERAL ambapo
hadi jana hali yake haikuwa mbaya sana leo ndio
kafikwa na umauti.Endelea kufuatilia taarifa zetu
tutakujuza.


kwa tasnia ya muziki wa kizazi kipya
nchini.
Mwanamuziki wa kizazi kipya nchini Tanzania
Moses Bushagama maarufu kwa jina la Mez B
ambaye alikuwa muimbaji katika kundi la Chamber
Squard,inaelezwa kuwa amefariki Dunia leo asubuhi
wakati amelazwa katika hospitali ya mwananchi
mjini Dodoma akipatiwa matibabu.
Akizungumza baada ya kupigiwa simu Dada wa Mez
B amethibitisha kifo cha kaka yake ambapo
amesema ni muda hivi amekuwa akisumbuliwa wa
homa pamoja na tatizo la kuishiwa Damu na hivyo
walimpeleka katika hospitali ya GENERAL ambapo
hadi jana hali yake haikuwa mbaya sana leo ndio
kafikwa na umauti.Endelea kufuatilia taarifa zetu
tutakujuza.


Jumatatu, 16 Februari 2015

Waziri wa wizara ya uchukuzi amemsimamisha kazi kwa muda usiojulikana kaimu mkurugezi

Waziri wa wizara ya uchukuzi amemsimamisha
kazi kwa muda usiojulikana kaimu mkurugenzi
mkuu wa mamlaka ya bandari madeni kipande ili
kupisha uchunguzi wa tuhuma mbalimbali
zinazomkabili ikiwemo ukiukwaji wa taratibu za
manunuzi.
Tuhuma nyingine zinazomkabili ni mahusiano
yasoyoridhisha kati ya uongozi wa mamlaka hiyo
na wadau wake muhimu ambapo pia mara kadhaa
imetokea bodi inapopitisha mazabuni yeye
huchelewesha barua, huku tume ya watu sita
ikiundwa kuchunguza tuhuma hizo na Bw Awadhi
Massawe akiteuliwa kushika wadhifa huo.
Wakati huohuo kamati ya bunge ya hesabu za
serikali na mashirika ya umma PAC imeitaka
serikali kujenga bomba la kusafirisha mafuta
kwenda mikoani ili kuepusha uharibifu wa barabara
unaofanywa na malori yanayosafirisha mafuta ikiwa
ni pamoja na kuwa na matenki makubwa ya umma
ya kuhifadhia mafuta ili kupunguza msongamano
wa meli za mafuta baharini.
Mwenyekiti wa kamati hiyo Mh Zitto Kabwe ametoa
wito huo mara baada ya kutembelea na kukagua
eneo linalotumika kupokelea mafuta ambapo pia
wameishauri serikali kufikiria chanzo maalum cha
mapato kwa ajili ya ujenzi wa reli akitolea mfano
nchi ya Kenya ambayo hutumia mapato ya kodi za
bidhaa zinazotoka nje kupanua reli yao.
Akijibu maswali mbalimbali ya wajumbe wa kamati
hiyo kaimu mkurugenzi wa TPA Bw Awadhi
Massawe amesema asilimia 90 ya mizigo yote
inayotoka bandarini inasafirishwa kwa njia ya
barabara hivyo ni vyema serikali ikaweka mkazo
kwenye ujenzi wa mabomba hayo pamoja na
uimarishwaji wa miundombinu ya reli huku
mwakilishi kutoka tra akielezea utaratibu
unaotumika kukusanya kodi.


Mkoani tanga hofu ikitanda kufwatia sakata la ugaidi

Jeshi la polisi mkoani Tanga limesema linafanya
uchunguzi wa kina kuhusu tukio la vikundi vya
uhalifu kuweka kambi katika mapango ya mleni maji
moto yaliyopo eneo la amboni jijini Tanga kufuatia
sehemu kubwa ya wananchi kulihusisha tukio hilo
na vitendo vya ugaidi hatua ambayo inawapa hofu
wananchi kuhusu usalama wao.


Jumamosi, 7 Februari 2015

Wanamgambo 27 wauawa misri



Wanamgambo 27 wa kiislamu wameuawa kwenye oparesheni kubwa iyoendeshwa na jeshi la Misri katika eneo la Sinai Kaskazini.
Taarifa zinasema kuwa ndege za helikopta zilitumiwa kuwalenga wapiganaji hao ambao wametangaza kulitii kundi la Islamic State.
Ripoti zinasema kuwa wanajeshi wa Misri baadaye waliwaua kwa kuwapiga risasi wanachama 20 wa kundi hilo.
Kundi hilo linasema kuwa liliwavizia wanajeshi wa Misri mwezi uliopita ambapo zaidi ya wanajeshi 30 waliuawa.



Posted via Blogaway


Kamati ya nidhamu ya TFF yatoa hukumu Kamati ya Nidhamu ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) imetoa adhabu kwa watu tisa wakiwemo viongozi, wachezaji na kocha mmoja kwa kupatikana na hatia ya makosa ya kinidhamu.

 Katika kikao chake kilichofanyika juzi (Februari 3 mwaka huu) jijini Dar es Salaam, Kamati hiyo imewafungia mwaka mmoja viongozi wawili wa Chama cha Mpira wa Miguu wa Wanawake Tanzania (TWFA) Mkoa wa Mwanza kwa kuwashawishi wachezaji wa Mwanza Queens kugomea uamuzi halali. Sophia Tigalyoma (Mwenyekiti) na Katibu wake Hawa Bajanguo walitiwa hatiani kwa kuwashawishi wachezaji kugomea uamuzi wa Kamati ya Mpira wa Miguu wa Wanawake ya TFF kutupa rufani yao dhidi ya Kigoma. Kocha wa Polisi Tabora, Eliakim Christopher amefungiwa mechi kumi na kupigwa faini ya sh. 300,000 kwa mujibu wa Kanuni ya 39(2) ya Ligi Daraja la Kwanza (FDL) baada ya kutiwa hatiani kwa kumtukana refa wakati wa mechi kati ya timu yake na Panone FC iliyochezwa mjini Moshi. Wachezaji wa JKT Oljoro FC, Dihe Makonga, Swaleh Idd Hussein, Ramadhan Mnyambegu na nahodha Shaibu Nayopa wamefungiwa mechi tatu na faini ya sh. 300,000 kila mmoja kwa kuzingatia kanuni ya 36(10) ya FDL kutokana na kufanya vurugu kwenye mechi kati yao na Burkina Faso iliyochezwa mjini Morogoro. Mtunza Vifaa (Kit Man) wa JKT Oljoro FC, Eliud Mjarifu amefungiwa miezi sita na kupigwa faini ya sh. 200,000 kwa kumpiga Kocha wa Burkina Faso, CR Mwakambaya kwenye mechi kati ya timu hizo iliyofanyika Uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro. Pia Mjarifu amepewa onyo kali na kutakiwa kutorudia tena kutenda kosa, kwani hata mwenendo wake wakati wa shauri hilo ulionyesha utovu wa nidhamu mbele ya Kamati. Naye Mtunza Vifaa wa Rhino Rangers FC, Albert Mbuji amefungiwa miezi sita na faini ya sh. 200,000 kwa kupatikana na hatia ya kuwatukana na kugomea uamuzi wa marefa kwenye mechi dhidi ya Polisi Dodoma. Adhabu hizo zimetolewa kwa mujibu wa kanuni ya 40(2) ya FDL. Kamati hiyo imeondoa malalamiko dhidi ya Ofisa Habari wa klabu ya Ruvu Shooting, Masau Bwire kwa vile refa Israel Mujuni Nkongo ambaye ni mlalamikaji hakufika kwenye shauri hilo. Nkongo alimlalamikia Bwire akidai alitoa maneno yenye kuweza kuchochea chuki dhidi yake kwa waamuzi, kwani kupitia redio 100.5 Times FM, Bwire alidai refa huyo ndiye aliyeshinikiza kuondolewa kwa refa Mohamed Theofil kwenye ratiba ya Ligi Kuu ya Vodacom (VPL). Pia Kamati hiyo imemkuta bila hatia Kaimu Katibu Mkuu wa Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Singida (SIREFA), Gabriel Gunda ambaye TFF ilimlalamikia kuwa akiwa mtendaji mkuu wa chama hicho alishindwa kuhakikisha timu ya Singida inaingia uwanjani kucheza na Dodoma kwenye mechi ya Kombe la Taifa kwa Wanawake. Kamati ilikubaliana na utetezi wa Gunda kuwa, jukumu la timu hiyo lilikuwa mikononi mwa viongozi wa TWFA Singida, na tayari SIREFA kupitia Kamati yake ya Nidhamu ilishatoa adhabu kwa viongozi wa timu hiyo kutokana na kitendo hicho. Nayo malalamiko ya Polisi Tabora FC kutaka mechi yao dhidi ya Toto Africans FC irudiwe kwenye uwanja huru (neutral ground) kwa madai ya kuchezeshwa zaidi ya muda unaotakiwa, na kutokuwepo ulinzi wa kutosha kwenye Uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza yamekataliwa. Pia Kamati ya Nidhamu imeelekeza malalamiko ya timu za Mwadui FC na Polisi Mara FC dhidi ya Toto Africans kwa kumchezesha mchezaji Ladislaus Mbogo bila kuonyesha leseni yake yasikilizwe haraka na Bodi ya Ligi Kuu Tanzania (TPLB) kwa vile si ya kinidhamu. Wakati huo huo, Kamati ya Nidhamu inaendelea na kikao chake leo (Februari 5 mwaka huu) kusikiliza malalamiko mengine ya kinidhamu yaliyofikishwa mbele yake. 


MBUNGE AUWAWA NCHIN KENYA


PICHA HAPO JUU NIGARI LA MBUNGE⇧

Mbunge mmoja ameuawa kwa kupigwa risisi kwenye mji mkuu wa kenya Nairobi.
Ripoti za polisi zinasema kuwa mbunge huyo wa Kabete, eneo lililo nje kidogo ya mji wa Nairobi aliuawa na watu wasiojulikana usiku wa kuamkia leo.
Walinzi wake wawili,dereva pia nao wameuawa.
Polisi wanasema kuwa watu waliokuwa na silaha walilifuata gari la mbunge huyo kutoka eneo la Westlands kabla ya kulimiminia rasasi ndani ya mji wa Nairobi.

Ijumaa, 6 Februari 2015

CUF ya wahimiza wananchi kujiandikisha katika Daftari la kudumu la wapiga kura na kuunga mkono maazimio ya UKAWA.


Chama cha wananchi CUF katika mikoa ya lindi na
mtwara, kimewataka wananchi wa mikoa hiyo
kujitokeza kwa wingi kujiandikisha katika Daftari la
kudumu la wapiga kura, ili waweze kushiriki
kikamilifu katika uchaguzi mkuu ujao.
Rai hiyo imetolewa na viongozi wa chama hicho
katika mkutano wa hadhara mjini lindi, uliofanyika
kwa malengo ya kuwaelimisha wananchi juu ya
umuhimu wa kushiriki katika zoezi la kujiandikisha
katika daftari la kudumu la wapiga kura.
Viongozi wa chama cha wananchi CUF kanda ya
kusini wakizungumza na wananchi katika eneo la
sabasaba mjini lindi wametumia fursa hiyo
kuwaomba wananchi kujitokeza kwa wingi
kujiandikisha katika daftari la kudumu la wapiga
kura ili kuweza kupata haki yao ya kikatiba ya
kushiriki katika zoezi la uchaguzi mkuu mwaka
huu.
Aidha viongozi hao pia wametumia nafasi hiyo
kuwaomba wananchi kuunga mkono msimamo
uliotolewa na vyama vya upinzani vinavyounda
umoja wa katiba ya wananchi ukawa,wa kutoshiriki
katika zoezi la kupigia kura rasimu
inayopendekezwa mpaka hapo muda na elimu ya
kutosha vitakapotolewa kwa wananchi.
Hata hivyo #uhondo ikataka kujiridhisha iwapo wananchi
katika maeneo hayo wanauelewa wa kutosha
kuhusu elimu ya katiba, ambapo wamedai kuwa
licha ya kutoifahamu rasimu pendekezwa
inayozungumziwa sasa, hata hiyo ya zamani pia
hawajahi kuitia machoni.