Wanamgambo 27 wa kiislamu wameuawa kwenye oparesheni kubwa iyoendeshwa na jeshi la Misri katika eneo la Sinai Kaskazini.
Taarifa zinasema kuwa ndege za helikopta zilitumiwa kuwalenga wapiganaji hao ambao wametangaza kulitii kundi la Islamic State.
Ripoti zinasema kuwa wanajeshi wa Misri baadaye waliwaua kwa kuwapiga risasi wanachama 20 wa kundi hilo.
Kundi hilo linasema kuwa liliwavizia wanajeshi wa Misri mwezi uliopita ambapo zaidi ya wanajeshi 30 waliuawa.
Posted via Blogaway
Jumamosi, 7 Februari 2015
Wanamgambo 27 wauawa misri
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni