Jumatatu, 26 Januari 2015

Mh dk magufuri amesema kwamba hata kama serikali itajenga barabara nyingi kiasigani


Waziri wa ujenzi Mh Dk John Magufuli amesema
hata kama serikali itajenga barabara nyingi kiasi
gani lakini barabara hizo zikigeuza kuwa ni
sehemu ya kufanyia biashara tatizo la foleni katika
jiji la Dar es Saalam halitakwisha hivyo ameagiza
watu wote wanaoafanya hivyo hatua kali dhidi yao
zichuliwe.
Mh Magufukli ameyasema hapo katika zira yake ya
kukagua ujenzi wa barabra mbalimbali katika jini la
Dar es Salaam ambapo amesema inashangaza
kona kuwa mabilioni ya fedha yanatumika kujenga
barabara tena kwa kodi a wananchi huku baadhi
ya watu wanazihujumu hizo barabra.
Kwa upande wake mkuu wa mkoa wa Dar es
Salaam Bw Said Meki Sadik ameziagiza
halmashauri zote za mkoa kuhakisha kuwa katika
bajeti ya mwaka huu wahakishe wanaongeza bajeti
ya ujenzi wa barabara na kama hawatafanya hivyo
hatozipitisha bajeti zao.
Partick Mfugale ni mtendaji mkuu wa wakala wa
barabara nchini amesema miradi mingi inakwenda
vizuri ila changamoto kubwa ni serikali kuchelewa
kutoa fedha tatizo ambalo linachelewesha ujenzi
wa barabara.
Akizungumza katika uzinduzi huo mbunge wa
ubungo Mh Johm Mnyika amepongeza hatua
iliyofikiwa na kusema kuwa kama barabra hizo
zitakamilika zitasaidia kupunguza msongamano
wa foleni huku mwenyekiti wa CCM mkoa Dar es
Salaam Mh Ramadhnai Madabida akiahidi kuibana
serikali katika kutekeleza ahadi zake.

 uhondoleo.blogsport.com 

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni