Jumamosi, 24 Januari 2015

RAIS ATANGAZA MAWAZILI WAPYA 8


Rais Jakaya kikwete  ametangaza
mabadiliko katika baraza lake la mawaziri.
Rais amewateua mawaziri wanane wapya pamoja
na manaibu watano.
Tangazo hilo lilifanywa na katibu katika ikulu ya
rais balozi Ombeni Sefue.
Mabadiliko hayo yanajumuisha wadhfa wa waziri
wa nishati na kawi wa Profesa Muhongo ambaye
amejiuzulu mapema leo pamoja na wadhfa wa
waziri wa ardhi ambao uliwachwa wazi baada ya
kupigwa kalamu kwa Anna Tibaijuka.
Mawaziri hao wawili wanahusishwa na kashfa ya
ufisadi ambayo ilimshinikiza mwanasheria mkuu
pia kujiuzulu.Nafasi ya Profesa Muhongo
imechukuliwa na aliyekuwa naibu wa waziri wa
ardhi, George Simbachawene
Rais Kikwete amewaapisha mawaziri hao wapya hii
leo katika tangazo lililorushwa hewani na runinga
ya taifa moja kwa moja.
Hii ndio orodha ya mawaziri walioteuliwa
MAWAZIRI
George Simachawene waziri wa nishati na madini
Mary Nagu- waziri wa nchi [afisi ya rais]
mahusiano na uratibu
Christopher chiza -waziri uwezeshaji na uwekezaji
Harisson Mwakyembe[waziri wa ushirikiano wa
afrika mashariki]
William Lukuvi -waziri wa ardhi nyumba na
makaazi
Steven Wasira -waziri wa kilimo chakula na
ushirika
Samwel Sita -waziri wa uchukuzi
Jenista Muhagama -waziri wa nchi ofisi ya waziri
mkuu sera uratibu na bunge
MANAIBU WAZIRI
Stephen Masele -naibu waziri afisi ya makamu wa
rais muungano
Angela Kariuki -naibu waziri wa ardhi nyumba na
makaazi
Ummi Mwalimu- naibu waziri wa katiba na sheria
Anna Kilango naibu waziri wa elimu na mafunzo ya
kiufundi
Charles Mwijage-naibu waziri wa nishati na madini

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni